<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<!-- generator="FeedCreator 1.7.2" -->
<rss version="2.0" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom">
    <channel>
        <atom:link href="http://haleluyaministry.yolasite.com/news.rss" rel="self" type="application/rss+xml" />
        <title>news</title>
        <description>news</description>
        <link>http://haleluyaministry.yolasite.com/news.php</link>
        <lastBuildDate>Fri, 05 Jun 2026 20:57:54 +0100</lastBuildDate>
        <generator>FeedCreator 1.7.2</generator>
        <item>
            <title>Mafundisho ya neno la Mungu</title>
            <link>http://haleluyaministry.yolasite.com/news/mafundisho-ya-neno-la-mungu</link>
            <description>

&lt;h2&gt;&lt;br&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;&lt;/span&gt;&lt;/h2&gt;&lt;h2&gt;&lt;span style=&quot;background-color: rgb(255, 0, 255);&quot; tag=&quot;span&quot; class=&quot;yui-tag-span yui-tag&quot;&gt;HABARI MPYA, Februari 21, 2012&lt;/span&gt;&lt;br&gt;&lt;/h2&gt;&lt;b style=&quot;background-color: rgb(128, 255, 0); font-size: 18px;&quot;&gt;&lt;span style=&quot;background-color: rgb(255, 0, 0); font-size: 18px;&quot; tag=&quot;span&quot; class=&quot;yui-tag-span yui-tag&quot;&gt;WASIOSIKIA NA WASIOONGEA (VIZIWI NA MABUBU) WAONGEA NA KUSIKIA&lt;/span&gt;&lt;/b&gt; &lt;br&gt;&lt;br&gt;Mabinti wawili wenye umri kati ya miaka 30 na 28 wameponywa baada ya kufanyiwa maombi katika Huduma ya Haleluya. Mabinti hao ambao walikuwa hawasikii wala kuongea walifunguka katika ibada ya Jumapili ya tarehe 19 Februari 2012. Mary na Martina ni wakazi wa Mabibo Dar es Salaam na ndio waliopokea muujiza wa uponyaji.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Baada ya kufunguliwa, Mary alijitambulisha kuwa alizaliwa Songea, Mkoa wa Ruvuma na mwenzake, Martina yeye ni mzaliwa wa Geita, Mkoa wa Mwanza. Wadada hawa walimshukuru sana Mungu kwa uponyaji kwani wamekuwa katika hali hiyo kwa miaka mingi.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Washirika wa Kanisa la Haleluya walilipuka kwa shangwe kubwa baada ya kusikia wadada hawa wakitaja majina yao na kusema kuwa wanakaa Mabibo.&lt;br&gt;&lt;br&gt;Wakati huo huo, mwaka jana dada mmoja toka Iringa aliyejulikana kwa jina la Twendeni, aliponywa ukipofu. Kwa sasa binti huyo ambaye amekuwa kipofu kwa miaka mingi sasa ni mzima na taarifa iliyopatikana toka Iringa ilisema kwambna kwa sasa anataraji kurudi shuleni. Awali ilijulikana kwamba binti huyo alipofuka akiwa kidato cha pili huko kwao Iringa. Kwa sasa angekuwa amemaliza kidato cha sita. &lt;br&gt;&lt;br&gt;Tunamshukuru sana Mungu kwa uponyaji huu kwa maana neno linasema &quot;Njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha&quot; Mathayo 11:28.&lt;br&gt;&lt;br&gt;&lt;h2&gt;&lt;br&gt;&lt;/h2&gt;&lt;h2&gt;&lt;br&gt;&lt;/h2&gt;&lt;h2&gt;&lt;br&gt;&lt;/h2&gt;&lt;h2&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kufunga &lt;a class=&quot;&quot; href=&quot;http://www.heavensfamily.org/ss/pdf/tdmm_swahili/tdmm_swahili_26.pdf&quot;&gt;&lt;span style=&quot;text-decoration: none;&quot;&gt;&lt;img class=&quot;yui-img&quot; src=&quot;file:///C:/DOCUME%7E1/Costech/LOCALS%7E1/Temp/msohtml1/01/clip_image001.gif&quot; width=&quot;27&quot; border=&quot;0&quot; height=&quot;15&quot;&gt;&lt;/span&gt;&lt;/a&gt;&lt;/span&gt;&lt;/h2&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kufunga ni tendo la hiari la kuacha kula
chakula na kinywaji, au kuacha kinywaji, kwa kipindi fulani.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Biblia imeandika mifano mingi ya watu
waliofunga. Wengine waliacha kula vyakula &lt;i&gt;vyote &lt;/i&gt;na wengine waliacha kula
vyakula &lt;i&gt;fulani tu &lt;/i&gt;kwa muda wa mfungo wao. Mfano wa hili la mwisho ni ule
mfungo wa Danieli wa majuma matatu, ambao hakula “chakula kitamu … nyama wala
divai” (Danieli 10:3).&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Vile vile kuna mifano michache katika
Maandiko ya watu waliofunga kula chakula na maji, lakini aina hii ya mfungo
kamili si wa kawaida, na unatakiwa kuhesabiwa kuwa wa kiMungu ikiwa ulizidi
siku tatu. Kwa mfano: Wakati Musa alipokaa siku arobaini bila kula wala kunywa
chochote, alikuwa mbele za Mungu Mwenyewe mpaka uso wake uling’aa (ona Kutoka
34:28, 29). Alirudia mfungo wa siku arobaini tena, muda mfupi tu baada ya ule
wa kwanza (ona Kumbu. 9:9, 18). Hiyo mifungo yake haikuwa ya kawaida, na si
vizuri kwa yeyote kujaribu kuiga. Bila ya msaada wa Mungu, haiwezekani kwa mtu
kukaa zaidi ya siku chache bila maji. Kuishiwa maji mwilini husababisha kifo.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Hatari kwa afya si kukaa bila maji kwa muda
mrefu tu. Hata kuacha kula chakula kwa vipindi virefu huweza kuwa hatari pia,
hasa kwa watu ambao wana matatizo ya chakula tayari. Na hata wenye afya nzuri
wanapaswa kuwa makini ikiwa wanapanga kufunga kwa muda mrefu zaidi ya wiki
moja.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;h2&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kwa Nini Watu Wafunge? &lt;/span&gt;&lt;/h2&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kusudi la msingi la kufunga ni kujipatia muda
wa ziada ili kuomba na kumtafuta Bwana. Ukisoma Biblia, hakuna mahali ambapo
kufunga kunatajwa bila kuhusisha maombi. Hiyo inatufanya tuseme kwamba kufunga
bila kuomba ni kazi bure. Kwa mfano: Katika kitabu cha Matendo, tunasoma sehemu
mbili kuhusu kufunga, na kote maombi yanatajwa. Sehemu ya kwanza (ona Matendo
13:1-3), manabii na waalimu katika kanisa la Antiokia walikuwa “wakimfanyia
Mungu ibada na kufunga.” Walipofanya hivyo, wakapokea mafunuo ya kinabii, na
kwa sababu hiyo wakamtuma Paulo na Barnaba kwenda safari yao ya kwanza ya kimishenari. Katika sehemu
ya pili, Paulo na Barnaba walikuwa wanaweka wazee wa kusimamia makanisa mapya
huko Galatia.
Tunasoma hivi:&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika
kila kanisa na kuomba pamoja na kufunga, wakawaweka katika mikono ya Bwana
waliyemwamini (Matendo 14:23).&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Pengine katika mfano huu wa pili, Paulo na
Barnaba walikuwa wanafuata mfano wa Yesu, maana yeye aliomba usiku kucha kabla
ya kuchagua wale Thenashara (ona Luka 6:12). Maamuzi muhimu – kama
kuchagua viongozi wa kiroho – yanahitaji kuombewa mpaka mtu awe na uhakika
kwamba ameongozwa na Bwana. Kufunga kutatoa nafasi nzuri zaidi ya kuomba kwa
habari hiyo. Ikiwa Agano Jipya linashauri wanandoa kuacha kushirikiana kimwili
ili kuongeza muda wa kuomba (ona 1Wakor. 7:5), basi ni rahisi kuelewa jinsi
ambavyo kuacha chakula kwa muda kutafanikisha kusudi hili hilo.&lt;a class=&quot;&quot; href=&quot;http://www.heavensfamily.org/ss/swahili/tdmm_swahili/tdmm_swahili_26#_ftn1#_ftn1&quot; title=&quot;&quot;&gt;[1]&lt;/a&gt;&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Basi, tunapohitaji kuomba ili Mungu
atuelekeze kwa maamuzi muhimu ya kiroho, kufunga ni kitu cha kufanya. Maombi
kwa ajili ya mahitaji mengine yanaweza kufanywa kwa muda mfupi sana. (Mfano: Hatuhitaji kufunga ili kuomba
sala ya Bwana.) Maombi kwa ajili ya uongozi yanachukua muda mrefu zaidi kwa
sababu ya ugumu wetu wa “kusikia sauti ya Mungu.” Kupata uhakika kuhusu
maongozi kunaweza kuhitaji maombi ya muda mrefu, na hapo ndipo kufunga
kunapokuwa na faida.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;h2&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Sababu Mbaya Za Kufunga &lt;/span&gt;&lt;/h2&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kwa kuwa tumetoa sababu za kiMaandiko za
kufunga katika Agano Jipya, hebu tutazame sababu zisizokuwa za Maandiko za
kufunga.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kuna watu ambao wanafunga kwa matumaini
kwamba itaongeza uwezekano wa Mungu kujibu maombi yao. Sivyo, maana Yesu alituambia kwamba
msingi wa kujibiwa maombi ni imani, si kufunga (ona Mathayo 21:22). Tukumbuke
kwamba kufunga hakumbadilishi Mungu hata kidogo. Yeye yuko vile vile kabla
hatujafunga, na tunapofunga, na baada ya kufunga. Kufunga si njia ya “kumbana
Mungu” au namna ya kumwambia, “Lazima ujibu maombi yangu la sivyo nitafunga
mpaka nife!” Huko si kufunga KiBiblia – huko ni kugomea chakula! Kumbuka Daudi
alifunga na kuomba kwa siku kadhaa ili yule mtoto wake mgonjwa waliyezaa na
Batsheba asife, lakini mtoto alikufa kwa sababu Mungu alikuwa anamwadhibu.
Kufunga hakukubadilisha hali yake. Daudi hakuwa anaomba kwa imani kwa sababu
hakuwa na ahadi yoyote ya kusimamia. Alikuwa anafunga na kuomba kinyume cha
mapenzi ya Mungu, kama matokeo
yalivyo-onyesha.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kufunga si sharti la kupata uamsho, kama wengine wanavyofikiri. Katika Agano Jipya, hakuna
mfano wa yeyote akifunga kwa ajili ya uamsho. Badala yake tunawaona mitume
wakimtii Yesu kwa kuhubiri Injili. Kama mji
haukupokea, walimtii Yesu tena, wakikung’uta mavumbi miguuni pao na kusafiri
hadi mji uliofuata (ona Luka 9:5; Matendo 13:49-51). Hawakuketi mahali na
kufunga, wakisubiri uamsho.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Vile vile kufunga si njia ya “kutiisha mwili”
maana shauku ya kula chakula ni kitu halali na wala si dhambi. Angalia katika
Wagalatia 5:19-21 uone orodha ya “tamaa za mwili.” Ila, kufunga ni zoezi la
kujitawala – au kiasi – na hiyo ni sifa inayohitajika ili kuenenda katika Roho,
si katika mwili.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kufunga kwa kusudi la kuboresha kiroho chako
au kutangaza jinsi unavyompenda Mungu ni kupoteza wakati na ni ishara ya
unafiki. Hiyo ndiyo sababu iliyowafanya Mafarisayo kufunga, na Yesu aliwasema
kwa hilo (ona
Mathayo 6:16; 23:5).&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Watu wengine hufunga ili kumshinda Shetani. Hilo nalo si Maandiko. Maandiko
yanatuahidi kwamba tukimpinga Shetani kwa imani katika Neno la Mungu,
atatukimbia (ona Yakobo 4:7; 1Petro 5:8, 9). Hapo kufunga hakupo.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Lakini, si Yesu alisema kwamba kuna mapepo
mengine yasiyotoka “isipokuwa kwa kufunga na kuomba”?&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Maneno hayo yalisemwa kwa habari ya kumweka
mtu huru kutokana na pepo ililokuwa limempagaa, si kwa habari ya mwamini
anayehitaji kupata ushindi juu ya mashambulizi ya Shetani kinyume chake.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Swali: Je, maneno ya Yesu hayaonyeshi kwamba
tunaweza kupata mamlaka makubwa zaidi juu ya mapepo kwa kufunga?&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kumbuka kwamba wakati baadhi ya wanafunzi wa
Yesu walipomwuliza kwa nini wao walishindwa kumtoa mvulana fulani pepo, kwanza
alijibu kwamba ni kwa sababu ya imani yao
ndogo (ona Mathayo 17:20). &lt;i&gt;Pengine&lt;/i&gt; aliongezea, “Namna hii haiwezeani
isipokuwa kwa kufunga na kuomba” (Mathayo 17:21), lakini maneno hayo huenda
hayakuwepo katika Injili ya Mathayo – yaliongezwa baadaye.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Ila – hata kama Yesu alisema maneno hayo,
tutakosea sana
kuamua kwamba kufunga kunaweza kuongeza mamlaka ya mtu juu ya mapepo. Kama Yesu
atampa mtu mamlaka juu ya mapepo kama
alivyofanya kwa wanafunzi Wake kumi na mbili (ona Mathayo 10:1), basi anayo, na
kufunga hakuwezi kuyaongeza. Ila, kufunga kunatoa muda zaidi wa kuomba na
kutafakari, na kwa njia hiyo kumwongezea imani katika mamlaka yake aliyopewa na
Mungu.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kumbuka kwamba kama
Yesu alisema maneno hayo tunayochambua, yalihusu &lt;i&gt;aina moja&lt;/i&gt; tu ya pepo.
Kufunga bado kungechukua sehemu ndogo sana
katika huduma ya ukombozi kwa ujumla, kama
basi kuna sehemu yoyote.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;h2&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Mkazo Kupita Kiasi Kuhusu Kufunga &lt;/span&gt;&lt;/h2&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kwa bahati mbaya sana,
baadhi ya Wakristo wameunda dini kwa habari ya kufunga, wakitoa mahali pakubwa sana katika maisha yao ya
Kikristo kwa jambo hilo.
Kufungwa hakutajwi hata mara moja katika nyaraka za Agano Jipya.&lt;a name=&quot;_ftnref2&quot;&gt;&lt;/a&gt;&lt;a class=&quot;&quot; href=&quot;http://www.heavensfamily.org/ss/swahili/tdmm_swahili/tdmm_swahili_26#_ftn2#_ftn2&quot; title=&quot;&quot;&gt;&lt;span style=&quot;&quot;&gt;[2]&lt;/span&gt;&lt;span style=&quot;&quot;&gt;&lt;/span&gt;&lt;/a&gt;&lt;span style=&quot;&quot;&gt;&lt;/span&gt; Hakuna
mafundisho yatolewayo kwa waamini kuhusu jinsi ya kufunga, au wafunge lini.
Watu hawatiwi moyo kufunga. Hii inatuonysha kwamba kufunga ni sehemu ndogo sana katika kumfuata
Yesu.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Inaonekana kwamba wakati wa agano la zamani
kufunga kulikuwa na mahali pakubwa zaidi. Mara nyingi kufunga kulihusisha na
wakati wa maombolezo – kama mtu akifa au wakati wa toba, na wakati wa maombi ya
dhati katika vipindi vya matatizo kitaifa au kibinafsi (ona Waamuzi 20:24-28;
1Sam. 1:7, 8; 7:1-6; 31:11-13; 2Sam. 1:12; 12:15-23; 1Waf. 21:20-29; 2Nyakati
20:1-3; Ezra 8:21-23; 10:1-6; Nehemia 1:1-4; 9:1, 2; Esta 4:1-3, 15-17; Zaburi
35:13, 14; 69:10; Isaya 58:1-7; Dan. 6:16-18; 9:1-3; Yoeli 1:13, 14; 2:12-17;
Yona 3:4-10; Zekaria 7:4-5).&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Vile vile, Agano la Kale linafundisha kwamba
kuheshimu sana kufunga na kupuuza kutii amri za
muhimu zaidi kama vile kuwajali maskini, ni
makosa (ona Isaya 58:1-12; Zekaria 7:1-14).&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Bwana Yesu ambaye alifanya huduma Yake wakati
wa agano la zamani hawezi kusemwa kwamba yeye alitilia mkazo kufunga kupia
kiasi. Alishtakiwa na Mafarisayo kwa kutotilia mkazo wa kutosha (ona Mathayo
9:14, 15). Aliwasema wao kwa kutilia mkazo kupita kiasi (ona Luka 18:9-12).&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Lakini pia, Yesu alizungumza na wafuasi Wake
kuhusu kufunga, katika mahubiri Yake ya Mlimani. Aliwaagiza wafunge kwa sababu
sahihi, akionyeshakwamba aliwatazamia wafuasi Wake kufunga nyakati fulani
fulani. Pia aliahidi kwamba Mungu angewapa thawabu kwa sababu ya kufunga kwao.
Yeye Mwenyewe alifunga kwa kiasi fulani (ona Mathayo 17:21).&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;h2&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Mtu Afunge Muda Gani? &lt;/span&gt;&lt;/h2&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Mifungo yote ya siku arobaini iliyoandikwa
katika Biblia si ya kawaida. Tayari tumetazama habari za Musa na mifungo yake
miwili ya siku arobaini, akiwa mbele za Mungu. Eliya vile vile alifunga siku
arobaini, lakini kabla ya hapo aliletewa chakula na malaika (ona 1Waf. 19:5-8).
Pia, kuna mambo yasiyokuwa ya kawaida kuhusu mfungo wa Yesu wa siku arobaini.
Yeye aliongozwa na Roho Mtakatifu kiajabu sana
kwenda nyikani. Alipata majaribu yasiyo ya kawaida, kutoka kwa Shetani,
alipokaribia mwisho wa mfungo wake. Pia, alitembelewa na malaika alipomalizia
mfungo Wake (ona Mathayo 4:1-11).&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Ingawa inawezekana kwa watu wengine kufunga
kwa siku arobaini pasipo msaada wa Mungu, wengi wanaweza kuwa wanahatarisha
afya zao. Mifungo ya siku arobaini si kawaida ya KiBiblia.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Mtu akiacha mlo mmoja kwa hiari yake mwenyewe
kwa kusudi la kupata wakati wak umtafuta Bwana, amefunga. Wazo kwamba kipimo
cha mifungo ni siku husika ni kosa.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Ile mifungo miwili katika Kitabu cha Matendo
tuliyokwisha taja (ona Matendo 13:1-3; 14:23) haikuwa ya muda mrefu. Yawezekana
ilikuwa ni mlo mmoja tu.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kwa kuwa kusudi la kufunga ni kupata muda wa
kumtafuta Bwana katika maombi kwa habari ya uongozi Wake, ushauri unaofaa ni
kwamba, funga muda wote unaohitaji, mpaka upate mwongozo unaohitaji kwa uwazi.
Kumbuka: Kufunga hakumlazimishi Mungu kusema na wewe. Kufunga kunaweza
kuboresha usikivu wako kwa Roho Mtakatifu. Mungu anasema na wewe ukifunga na usipofunga.
Ugumu tulio nao sisi ni kupambanua maongozi Yake na shauku zetu.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;h2&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Ushauri Muhimu&lt;/span&gt;&lt;/h2&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Kwa kawaida, kufunga huathiri mwili kwa njia
mbalimbali. Mtu anaweza kujisikia udhaifu, uchovu, kichwa kuuma, hali ya kutaka
kutapika, kujisikia kulewa, tumbo kuuma na kadhalika. Kama
mtu amezoea kunywa kahawa, chai, au vinywaji aina hiyo, baadhi ya mambo
yaliyotajwa hapo mbele yanaweza kutokana na kutotumia vitu hivyo katika muda wa
mfungo. Kama ni hivyo, ni vizuri kwa watu kama
hao kuanza kuacha kutumia vinywaji hivyo siku chache kabla ya mfungo wao. Mtu
akizoea kufunga mara kwa mara, atagundua kwamba inakuwa rahisi kufunga kadiri
anavyoendelea, japo atajisikia udhaifu fulani.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

&lt;p&gt;&lt;span style=&quot;font-size: 14pt;&quot;&gt;Mifungo imalizwe polepole, na kama mfungo
ulikuwa mrefu, basi mtu awe makini sana
kwamba anamalizaje. Kama tumbo la mtu
halijasaga chakula kigumu kwa muda wa siku tatu, si vizuri kwake kufungua kwa
kula vyakula vigumu. Anapaswa kuanza na vyakula rahisi kusagwa – au vyepesi.
Mifungo mirefu inahitaji muda mrefu zaidi kwa tumbo kuanza kuzoea vyakula tena,
lakini ukiacha mlo mmoja au miwili huna haja ya kipindi kirefu cha kumaliza
mfungo.&lt;/span&gt;&lt;/p&gt;

</description>
            <pubDate>Wed, 22 Feb 2012 08:33:49 +0100</pubDate>
        </item>
    </channel>
</rss>
